Takriban magaidi 20 na askari watatu waliuawa katika shambulizi mbili dhidi ya vituo vya jeshi huko Burkina Faso



Takriban magaidi 20 na askari watatu waliuawa katika shambulizi mbili dhidi ya vituo vya jeshi huko Burkina Faso, jeshi la nchi hiyo lilisema hapa katika taarifa ya Jumanne.

Mashambulio hayo yalilenga vituo vya kijeshi karibu usiku wa manane katika eneo la kaskazini la Banh na maeneo ya kaskazini magharibi mwa Toeni, kulingana na taarifa hiyo.
Mapema Jumapili, watu wenye silaha walishambulia waabudu kwenye kanisa moja, na kuwacha watu 14 wakiwa wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mkoa wa Mashariki karibu na mpaka na Niger.

Comments