USHUHUDA WA KWELI WA KICHAWI A:4-6

 

USHUHUDA WA KWELI WA KICHAlWI A:4-6




USHUHUDA WA KWELI WA KICHAWI A-4



Kuna jamaa walikuwa wanatoka dar kuelekea Mtwara,wakiwa njiani wakafika Lindi maeneo ya mandawa kuna kimlima hivi gari ikazingua kitu kidogo cha kurekebisha waendelee na safari mmoja wao akabanwa na haja ndogo akasogea akajisaidia basi tenngeneza gari likagoma.Dereva akapigiwa simu na dereva mwenzake akamueleza mahali walipo huyo dereva akasikitika aisee mmeharibikiwa hapo msala.

Gari likagoma ikabidi walale saa nane usiku wakashangaa dogo kama ana miaka 6 akatokea akasimama mbele ya ile gari akacheka sana Kwa nguvu akapotea jamaa uoga ikabidi wachune Tu ndani ya gari wanajisaidia kwenye chupa saa 12 asubuhi akaja jamaa kama chizi hivi akawa anaizunguka ile gari akasikitika anaongea mmepata tabu sana anazunguka tu, akaondoka akaja mbibi akasimama akaawangalia akaondoka kukawa kumekucha sasa wanapiga hesabu wafungue kifaa kilicho haribika wapeleke Kwa fundi,mmoja wao akataka kujisaidia tena ikatokea sauti ya mzee hakuna kujisaidia hapo ondokeni haraka huyo mzee akatokea wakamwambia gari ni mbovu akasema gari sio mbovu ondokeni dereva kuwasha gari nzima wakaendelea na safari kumbe kosa ni jamaa alivyojisaidia bwana.

USHUHUDA WA KWELI WA KICHAWI A-5

2010 nipo ndani ya fuso, natokea Ifakara kwenda dsm. Kufika Maseyu mida kama saa 8 usiku dereva akapaki, akasema amechoka anapumzika kidogo. Akatuambia saa 10 tumwamshe tuanze safari.

Sijui kama ni uchawi au ni nini, tulipitiwa na usingizi mzito, na wote, tulikuwa watatu tuliota ndoto ya aina moja. TUNAPIGA MECHI. tumejipiga mabao wote, kuangali saa ni dk 20 tu zimepita. Nilichowaeleza wenzangu ndio walichoota. Mwanamke niloyeota namgonga ndio huyo huyo wenzangu walikuwa wakiota wanamgona.

Niliota vipele vya baridi kwa uoga. Tukaondoka kuendelea na safari. Tangu siku hiyo sipandi tena malori ya mzigo yanayosafiri usiku.
 
USHUHUDA WA KWELI WA KICHAWI A-6

Nishawahi sikia kisa kinachohusishwa na uchawi

Kuna masela wawili walienda kwa mganga ili wapate utajiri

Mganga akawapa dawa akawaambia wakaoge usiku makaburini na wakitoka mlangoni kwa mganga hawatakiwi kugeuka nyuma

Basi unaambiwa safari yao iliandamwa na misukosuko yakutisha, mara wasikie muungurumo wa simba akiwa nyuma yao na vimbwenga vingi lakini walijitahidi kukaza ili kutovunja sharti la kugeuka nyuma

Sasa ulipofika usiku majira ya saa 8 ikabidi waende makaburini kuoga ili kumalizia zoezi lao la mwisho ili wawe mamilionea

Walipofika makaburini wakavua nguo wote nakubakia uchi kisha wakapanda juu ya kaburi ili waoge

si unajua ukiwa katika ile mood flani hivi unaoga halafu umefumba na macho ili maji yasiingie machoni.

wakastukia tu paap! wameshikwa makalio kwa nyuma.

Aaah unaambiwa wote ilibidi wageuke nyuma kwa haraka huku wanakimbia na kupiga makelele

Kesho yake kijiweni wakaanza kulaumiana "aaah wewe ndiye ulizingua, we ungekausha bila kupiga mikelele mi nisingechochora kwani kushikwa tako kitu gani bwana" yani leo nisingekua nakunywa kahawa hapa ningekua nimejikoki huko kwenye hotel zinazotambulika na dunia"

FUATILIA MUENDELEZO WA VISA HIVI A:1-30, B:1-30, C:1-30

Comments