USHUHUDA WA KWELI WA KICHAWI A:25-27
USHUHUDA WA KWELI WA KICHAWI A-25
ilikuwa 2002,tunatoka dar tunakwenda mkoa wa kigoma kwa wanojua bara bara enzi hizo wanajua ni jinsi gani kulikuwa na majambazi hasa ndani ya mapori ya Tabora,bahati haikuwa yetu mida ya saa 5 usiku wakati tupo road tukakuta bara bara imewekwa bonge la gogo mzee akataka kujitahid aligeuze ghafla walitokea watu wamebeba bunduki ndo kwa mara yangu ya kwanza kuone mtu kashka bunduki huku kajizungushia mkanda wa risasi mwilini bro wangu ile kuwaona tu akakata moto tuliokuwa hatujazmia tulikuwa watatu 3 mimi mzee na bimkubwa.
Tulichezea sana vitasa mzee alidhalilika mno mwisho wa siku walichukua mpka viatu nakumbuka viatu vyangu vya kitoto vya kuwaka taa,then wakaondoka mpka na gari tulikaa pale mpka saa 11 ndo tukapata msaada tukaenda polisi but hawakuwa na msaada mzee akapiga simu kigoma ikatumwa nauli tukaenda moja kwa moja mpka kwa baba yake(means babu),sasa babu yeye kila alivyokuwa anahadithiwa alikuwa anacheka mno hasa akimuangalia bro na ujanja wake ote et kazimia,upande wa baba yeye alikuwa na hasira mno alichokuwa anataka yeye ni wale watu awashikishe adabu hata kufa wafe basi ilivyofika usiku tukaelekea sehemu fulani inaitwa ujiji kwa mzee fulani alikuwa anaitwa juma njemba.
Nadhani kwa watu wa kigoma wanaweza kuwa wanamjua,akaelezewa kila kitu akasema hicho ni kitu kidogo sana,huku na yeye anacheka kisha akasema kuwa pale kwake kuna mbuzi alimchinja sababu ya sherwhe ya mwanae hvyo itatubidi tumtafutie mbuzi mwengne amreplace ili iwe kama malipo yake baba akakubali,kilichofata akawaita wajukuu zake walete (ubumba) ni udongo fulani hivi wa mfinyanzi kisha akawa anatengeneza kimdoli kidogo cha udongo kama vile vya kitoto toto,baada ya kukitengeneza akaanza kukiandika maneno yake kisha akakisimamisha chini,then akaanza kuongea maneno yake aliongea sana baada kama ya saa 1 akasema mtu yoyote ndani ya hichi chumba haruhusiwi kukimbia wala kupiga kelele kwani kwa kufanya hivyo ndo itakuwa kifo chake.
Basi aliendele kusema maneno yake ghafla yule mdoli pole pole alianza kukua na kuwa mkubwa pole pole,baada kama ya dakika arobaini alikuwa ni mkubwa kama binadamu mwenye mwili mkubwa alikuwa anamkono na kifua kikubwa na mrefu,kwa mara ya pili bro tena akazimia kwa mara ya pili mim mkojo ulishantoka natetemeka kama nmepatwa na dege dege,mwisho yule mdoli akaambiwa shtaka letu kisha akaambiwa nenda hivi vitu vinatakiwa leo leo,theb yule mtu akafungua mlango akatoka mbio alikuwa ni mwanaume lakini yupo uchi na ni mweusi tii kama mkaa mpka macho hakuwa na ichi kiini cheupe ye alikuwa na kiini cha moja kwa moja cha weusi,alivyoondoka tukaanza kumpepea na kumwagia maji bro alivyoshtuka yule mzee akatuambia kazi imeshakwisha kesho mtayapata majibu yenu.
Ilivyofika asubuhi tukapigiwa simu nakumbuka enzi hizo kulikuwa kuna buzz siyo hii tigo na hata simu zilikuwa za mezani,tukaambiwa kuwa kuna gari imepatikana Tabora yenye namba kama tuliyoripoti pamoja na vitu vingine,tukaanza safari na treni mpka tabora kufika kule tukakuta vitu vyetu na vingne vingi tu ila mzee alisema vyote vilikuwa vyetu hela zilikuwa kama 1m lakini zilipatikana 7m polisi hawakuchukua hata cent na hata walivyopewa walikataa kata kata hakikupotea hata kifungo kisha baada ya kuchukua tukaambiwa kuwa hao majambazi waliotuibia walikutwa msituni wakiwa wameuwawa wakasema wanahisi ni wanyama wakali ndo waliwauwa maana walikuwa wanaalama za meno makali milini mwao na kucha.
lakini wakashndwa kuelewa kama ni wanyama ndo waliwashambulia ni wanyama aina gani na kwanini hawakuwapiga hata risasi moja hao wanyama na wakati walikuwa na silaha nzito?Baada ya maelezo mengi mzee akawasha gari mpka kigoma stend ya kwanza mpka kwa yule mganga tulinunua mbuzi na zawadi nyingne nying lakini mzee aligoma hakutaka chochote zaidi ya mbuzi tu,basi tukampka mbuzi wake, akasema imebaki kazi moja tu na kazi yenyewe ni kumrudisha yule kiumbe(mdoli mtu)ili asitudhuru na sisi maana ni wetu hapo mdipo ilipokuwa mtihani maana kuna msharti mengi tulikosea plus kujisahau sasa akawa anatuandama sisi atuue dah kila mmoja nyumbani anaalama ya yule kiumbe yangu ni kungatwa skio na kula kipande nikipata mda ntawamalizia kisa changu but mpka leo mimi kwenda kwa waganga ni big no,but thanks god tulitoka salama
USHUHUDA WA KWELI WA KICHAWI A-26
kuna tukio lilitokea mkoa wa Rukwa wilaya na kijiji X.
watu wa kijiji hicho huwa jumapili wanapumzika kazi za shamba wanaenda kanisani kwani kijiji na mashamba yalipo kuna umbali na watu wengine wanalala huko huko kuna nyumba za muda ila jumapili wote wanakuwa kijijini.
basi kuna mama mmoja siku ya jumapili alikuwa anaenda shamba kuchuma mboga za majani, ili ufike shambani kuna msitu unapita. Wakati anakaribia kufika ule msitu akapishana na mbwa akiwa kasi anaelekea njia ya kijijini lakini yeye hakumjali kwani mbwa si kitu cha ajabu kwa kijijini.
akiwa anaendelea na safari yake katikati ya msitu akamuona mtu amekaa kwenye gogo akamsalimia na kuendelea na safari yake, kapiga hatua tatu akasikia yule mtu anamuita jina lake akageuka ili amuaangilie vizuri lakini kila akimuangalia yule mtu sura yake ikawa haileweki kama vile mtu anayejitazama kwenye kioo chenye ukungu.
yule mtu akaanza kumuuliza maswali yule mama:
mtu: huku akimtaja jina, unaenda wap?
mama:shambani.
mtu: kufanya nini?
mama: kutafuta mboga za majani.
mtu: wale samaki aliokuletea D kwa nini hujapika wale.
yule mama alishangaa jinsi alivyomuelezea mambo ya nyumbani kwake lakini akataka kumpuuza ili na safari lakini yule mtu alimwita tena safari hii kwa ukali, yule mama alipogeuka akashangaa baada ya kumuona yule mtu kawa wa ajabu zaidi kuliko mwanzo kwani sasa hata miguu yake utafikiri ni mtu anayeelea angani na sura isiyoeleweka kama ni mwanamke au mwanaume.
yule mtu akamuamuru yule mama kurudi alikotoka haraka huku akimwambia kwamba una bahati sana Leo. yule mama kwa hofu huku akitetemeka akaanza kukimbia kurudi kijijini kufika mwanzo wa msitu akapishana tena na yule mbwa akiwa kasi anarudi msituni.
USHUHUDA WA KWELI WA KICHAWI A-27
Miaka ya 1995 - 2000 kuna bwana mmoja alienda kwa mganga mahali fulani wilaya ya Njombe ili apate utajiri.
Masharti aliyopewa pamoja na dawa ni kulala katikati ya reli ya TAZARA usiku. Kwamba akisikia treni inakuja asiondoke aendelee kunuiza anataka utajiri wa kiwango gani.
E bwana ee, jamaa alisikia chuma kinaunguruma kama kilometa 5 kuja uelekeo wake. Sasa shida ikawa upande mmoja sijui ni moyo au ubongo au vyote vikaanza mjadala. Hiki ni kifo hapana huu ni utajiri.
Kukatisha maelezo jamaa aliyoka mbio baada ya kuinua kichwa na kuona kichwa cha treni kinasonga bila mjadala.
Aliamua kurudi kwao kijijini kukomaa na mpini wa jembe.
FUATILIA MUENDELEZO WA VISA HIVI A:1-30, B:1-30, C:1-30
Comments
Post a Comment